TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI


Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala anatoa taarifa kwamba, Manispaa ya imeanza zoezi la kukusanya takwimu za Wafanyabiashara wote na wamiliki wa nyumba na majengo katika Manispaa ya Ilala.

Lengo la zoezi hili ni kupata taarifa na takwimu sahihi za wakazi wetu na wafanyabiashara wote ndani ya Halmashauri ya manispaa ya Ilala ambazo zitatusaidia kuboresha huduma kwa wananchi wetu kutokana na idadi na mahitaji ya kila eneo.

Zoezi hili linaanza rasmi leo tarehe 08/04/2015 hadi  tarehe 08/07/2015 na litahusisha maeneo yote kuanzia katikati ya mji na meneo ya pembezoni.

Katika kipindi hicho watumishi wa Manispaa pamoja na waajiriwa wapya watapita maeneo yote kwa ajili ya kukusanya taarifa mbali mbali za kodi, tozo, leseni na malipo ya aina zote ikiwemo ushuru wa mabango ambapo mabango yote ndani ya Halmashauri ya Manispaa ya Ilala yatapimwa upya ili kujiridhisha na vipimo vya awali.

Maeneo mengine yatakayohusika ni ushuru wa masoko pamoja na ushuru wa kuzingira kwenye maeneo ya ujenzi.

Tunawaomba wananchi wetu na wafanyabiashara wote ndani ya manispaa ya Ilala kuwapa ushirikiano wafanyakazi wetu watakaopita katika maeneo yao. Pia tunawaomba wamiliki wa majengo kuacha taarifa zote muhimu ili kufanikisha zoezi hili; taarifa muhimu kwa wamiliki wa nyumba ni;

Ø Jina kamili la mmiliki

Ø Stakabadhi za malipo ya mara ya mwisho kama zipo

Ø Makadirio ya malipo yaliyofanywa na Manispaa kama yapo.  

Endapo kutajitokeza tatizo lolote tunawaomba wananchi na Wafanyabiashara kuwasiliana na ofisi za Watendaji wa Kata au Mitaa katika maeneo yao ili kupata ufafanuzi zaidi.

Pamoja na zoezi hili shughuli zote za kukusanya mapato, ulipaji wa tozo mbali  mbali  na ukataji wa leseni za biashara zitaendelea kama kawaida.


Imetolewa na,

Isaya M.Mngurumi

Mkurugenzi Halmashauri ya Manispaa ya Ilala



Chapisha Maoni

Mpya zaidi Nzee zaidi