TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI KWA BVR KITS OPERATORS NA WAANDISHI WASAIDIZI KWENYE ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA

Afisa Mwandikishaji Manispaa ya Ilala anawatangazia wenye sifa kujitokeza kuomba nafasi ya kazi ya kuwa BVR OPERATORS AU MWANDISHI MSAIDIZI kwenye zoezi la Uboreshaji wa Daftari la kudumu la Wapiga kura.
Sifa za Mwombaji
     i.        Awe ni Raia wa Tanzania
   ii.        Awe ni Mkazi wa Manispaa ya Ilala
  iii.        Awe anajua kusoma na kuandika
  iv.        Awe na Elimu ya Sekondari na kuendelea
    v.        Awe na Elimu ya kiwango cha cheti na kuendelea ya matumizi ya Kompyuta
  vi.        Awe ni Mkazi wa Kata anayoombea kufanya kazi
Jinsi ya kutuma maombi
     i.        Barua ya maombi iandikwe kwa mkono ikiwa na anuani kamili ya mwombaji na kuambatanishwa na vivuli ya vyeti.
   ii.        Mwombaji ataje Kata  anayoishi ambayo anaombea kufanya kazi hiyo
  iii.        Barua za maombi ziwasilishwe Ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala (Afisa Mwandikishaji) iliyopo katika makutano ya Barabara ya Mission na Sokoine kwa kutumia anuani ifuatayo;
Afisa Mwandikishaji,
Halmashauri ya Manispaa ya Ilala,
1 Mtaa wa Mission,
S.L.P 20950,
11883-Dar es Salaam.
N.B Siku ya mwisho ya kupokea maombi ni tarehe 19/06/2015 saa 9:30 alasiri.
Limetolewa na,

Chapisha Maoni

Mpya zaidi Nzee zaidi