ZUIO LA MAEGESHO YA MAGARI PEMBEZONI MWA BARABARA MAENEO YA KATIKATI YA JIJI NYAKATI ZA USIKU

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala anawatangazia wananchi na wakazi wa eneo la Kariakoo na katikati ya jiji kuwa, zoezi la Usafi wa Mazingira limekuwa likikwamishwa na magari yanayoegeshwa pembezoni mwa Barabara zote za katikati ya jiji nyakati za usiku.

Kwa Tangazo hili, Halmashauri ya Manispaa ya Ilala inatoa  Amri kwa Wakazi wa Eneo la katikati ya jiji kutokuegesha Magari pembezoni mwa barabara zote kuanzia saa 3.00 usiku.

Halmashauri itachukua hatua ya kuyafunga magari yote yatakayokutwa yameegeshwa  na Kuyaondoa pembezoni mwa barabara na kuyapeleka Karakana za Halmashauri na kutakiwa kulipia faini ya Sh.50,000/= kwa kila gari litakalokamatwa na kulazimika kulipia gharama za kvuta na kulaza gari.

"Manispaa ya Ilala bila Uchafu Inawezekana"

Limetolewa na,          



Isaya M. Mngurumi
Mkurugenzi Halmashauri ya Manispaa ya Ilala



Chapisha Maoni

Mpya zaidi Nzee zaidi