MKURUGENZI MANISPAA YA ILALA AKUTANA NA WAFANYABIASHARA NDOGO NDOGO WA KARIAKOO

Na: Hashim Jumbe
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala, Ndugu Isaya Mngurumi amekutana na Wafanyabiashara ndogo ndogo maarufu kama Wamachinga kutoka mitaa ya Kariakoo na kujadiliana changamoto mbalimbali wanazokabiliana nazo Wafanyabiashara hao na namna ya kuziondosha changamoto hizo.

Katika awamu ya pili ya majadiliano hayo, Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala alieleza mapendekezo ya mitaa itakayotumika kwa kufanyia biashara ndogo ndogo za Wamachinga pamoja na muda maalum wa kufanya biashara hizo, kama tiba ya kuondosha misongamano katika maeneo ya katikati ya Mji.
Mitaa iliyopendekezwa kutumika ni Kongo, Nyamwezi, Swahili na Sikukuu ambapo Mitaa ya Aggrey na Mkunguni haitatumika kwa biashara ndogo ndogo.  

Mitaa mingine ni Mchikichi, Mahiwa, Narun’gombe, Tandamti na Pemba ambapo Mtaa wa Livingstone hautatumika kwa biashara ndogo ndogo

Aidha, Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala aliagiza Mitaa hiyo itumike kuanzia saa 10:00 jioni hadi saa 3:00 usiku kwa siku za jumatatu hadi ijumaa, kuanzia saa 7:00 mchana hadi saa 3:00 usiku kwa siku za jumamosi na siku za jumapili kuanzia asubuhi hadi saa 3:00 usiku.

 
Mwenyekiti wa Kamati ya kuondoa usumbufu Manispaa ya Ilala, Mhe Saidi Abdallah Kitambuliyo ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Kiwalani akizungumza na Wamachinga katika mkutano wa pamoja uliofanyika kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala, Ndugu Isaya Mosses Mngurumi akitoa ufafanuzi wa Mitaa itakayotumika kwa Wafanyabiashara ndogo ndogo maarufu kama Wamachinga

Kiongozi wa Wafanyabiashara ndogo ndogo akieleza changamoto wanazokabiliana nazo wakati wa mkutano wa pamoja na Uongozi wa Manispaa ya Ilala


Wawakilishi wa vikundi mbalimbali vya Wamachinga waliohudhuria Mkutano wa pamoja na Viongozi wa Manispaa ya Ilala


Chapisha Maoni

Mpya zaidi Nzee zaidi