KAMATI YA FEDHA NA UONGOZI MANISPAA YA TEMEKE WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO MANISPAA YA ILALA

Na: Hashim Jumbe
Kamati ya Fedha na Uongozi kutoka Halmashauri ya Manispaa ya Temeke, leo imefanya ziara ya mafunzo kwenye Halmshauri ya Manispaa ya Ilala na kupata elimu namna gani Manispaa ya Ilala inavyokusanya mapato hususani kwenye eneo la masoko, ambapo Manispaa ya Ilala iliwaeleza namna bora ya ukusanyaji mapato kwenye masoko ikiwa ni pamoja na njia ya kutumia wawekezaji wa nje kukusanya ushuru.

Mbali na kuwa na shabaha ya kujifunza namna ya ukusanyaji mapato kwenye masoko, Ziara hiyo pia iliakisi mwanzo mwema wa ushirikiano kati ya Halmashauri hizo mbili.








                                    

Chapisha Maoni

Mpya zaidi Nzee zaidi