MSTAHIKI MEYA MANISPAA ILALA AZINDUA DARAJA LA KINYEREZI-BONYOKWA.

Na:Anjelina P.Mapunda

Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa  ya Ilala Mh.Charles Kuyeko akiambatana na Viongozi wengine wa Serikali pamoja na Watendaji wa Halmashauri katika uzinduzi wa daraja la Kinyerezi-Bonyokwa maeneo ya Kisiwani Jijini Dar es salaam.
Awali akizungumza katika hafla hiyo Mhandisi wa Manispaa ya Ilala ndugu Benjamin Maziku alisema daraja hilo linauwezo wakupitisha mzigo chini ya tani saba(7), lenye urefu wa mita 30  limejengwa kwa takribani mwaka mmoja na kugharimu Tsh.million 478 hadi kukamilika kwake. Ujenzi wa daraja hili umesua sua kwa siku nyingi kutokana na sababu mbali mbali lakini kutokana na usimamizi imara wa Mstahiki Meya wa Ilala Mhe. Charles Kuyeko sasa historia imebadilika 
Mstahiki Meya alipata fursa ya kuzindua daraja hilo linalounganisha Kata ya Bonyokwa na Kinyerezi, ambapo kukosekana kwa kivuko hicho ilikuwa ni kero kwa Wananchi wa kata hizo mbili na kuzuia mawasiliano pamoja na shughuli za maendeleo.
Katika uzinduzi huo Mstahiki Meya alipata fursa ya kuzungumza na Wananchi na  kuwasihi  kuwa Daraja hilo limejengwa na kodi zao,hivyo hawana budi kila Mwanachi awe mlinzi wa mwenzie katika kulinda daraja hilo ili kufanikisha gurudumu la maendeleo kusonga mbele katika kata hizo na Manispaa ya Ilala kwa ujumla.











Chapisha Maoni

Mpya zaidi Nzee zaidi