UBALOZI WA KUWAIT NCHINI TANZANIA WAKABIDHI VISIMA KUMI KWA SHULE ZA MSINGI MANISPAA YA ILALA

Na: Anjelina P. Mapunda
Ubalozi wa Kuwait nchini Tanzania ukishirikiana na Wadhamini kutoka Muslim Islamic Relief Organization, wamekabidhi  visima kumi (10) vya maji kwaajili ya shule za Msingi Manispaa ya Ilala ikiwa ni utekelezaji wa huduma ya maji kwa Wanafunzi

Awali Kaimu Afisa Elimu Msingi Bw. Hamis Mlangala alisema “visima  hivyo vyenye urefu zaidi ya mita 60 kwenda chini vimechimbwa katika Kata tofauti zilizoko  Manispaa ya Ilala, shule zilizonufaika na visima hivyo ni pamoja na Bwawani, Yombo, Umoja, Mwale, Kitunda, Jitihana, Serengeti, Mafuriko, Kombo na Vingunguti

 Naye Balozi wa Kuwait nchini Tanzania alisema Visima hivyo  vitatatua changamoto zilizokuwa zinawakabili Wanafunzi wa shule hizo. Pia aliongeza kwa kusema kuwa visima hivyo inabidi vitunzwe na kuwa na matumizi mazuri ya maji  kwa ajili ya manufaa ya vizazi vijavyo.













Chapisha Maoni

Mpya zaidi Nzee zaidi