MKUU WA WILAYA YA ILALA AZINDUA JENGO LA MAMA NA MTOTO ZAHANATI YA MSONGOLA, APOKEA NA VIFAA TIBA TOKA BENKI YA TIB

Na: Hashim Jumbe
Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Mhe. Sophia Mjema amezindua jengo la kutolea huduma ya Mama na Mtoto kwenye Zahanati ya Msongola, iliyopo Mtaa wa Yengayange pembezoni mwa Manispaa ya Ilala, huku ujenzi wa jengo hilo ukigharimu Jumla ya Shilingi Milioni 106.5 ambapo Shilingi Milioni 91.5 ni ufadhili kutoka Shirika la Kimataifa la Pathfinder na Shilingi Milioni 15 ni mchango wa Wananchi wa Kata ya Msongola.

Sanjari na uzinduzi wa Jengo hilo, lakini pia Mkuu huyo wa Wilaya ya Ilala alipokea na vifaa tiba vyenye thamani ya Shilingi Milioni 7 kutoka Benki ya TIB ili kuhakikisha huduma zinazotolewa kwenye Zahanati hiyo zina ubora unaostahili ikiwa ni pamoja uzazi bora na salama.

Vifaa tiba vilivyotolewa na Benki ya TIB ni pamoja na; Delivery beds-3 section with mattresses-2pcs, Delivery kit-superior quality 1 pc, Suction pump foot/hand operated 600 ml (twin) 1 pc, Blood pressure machine-Mobile Aneroid 1 pc, Blood pressure Machine-Digital 1 pc, Blood pressure machine-Aneroid 1 pc.

Zahanati hiyo ya Msongola iliyoanzishwa mwaka 1975 inahudumia Wakazi wapatao 24,461 kutoka maeneo yote ya Mtaa wa Yangeyange na Mitaa ya jirani kama vile Mbondole, Kitonga, Mvuleni na Mitaa ya Kisewe na Mbande iliyopo upande wa Manispaa ya Temeke, hivyo upatikanaji wa Jengo hilo pamoja na vifaa tiba utawarahisishia Wakazi wa maeneo hayo kupata huduma ya haraka
Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe. Sophia Mjema sambamba na Mbunge wa Jimbo la Ukonga Mhe. Mwita Waitara wakipokea vifaa tiba kutoka kwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya TIB Bw. Edward Lyimo wa kwanza kulia. Vifaa hivyo ni msaada kwaajili ya huduma za Mama na Mtoto
Wodi ya Mama na Mtoto kwenye Zahanati ya Msongola



Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe. Sophia Mjema akizindua rasmi jengo la Wazazi kwenye Zahanati ya Msongola


Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe. Sophia Mjema akishikana mkono na Mbunge wa Jimbo la Ukonga Mhe. Mwita Waita ikiwa ni ishara ya kuunga mkono kwa pamoja juhudi za kuleta maendeleo kwa Wananchi wa Manispaa ya Ilala bila itikadi ya aina yoyote
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Kimataifa Pathfinder-Tz, Dkt. Joseph Komwihangiro akizungumza mbele ya Mgeni rasmi ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Ilala wakati wa uzinduzi wa jengo la kutolea huduma ya Mama na Mtoto kwenye Zahanati ya Msongola. Pathfinder walichangia Shilingi Milioni 91.5 kwenye ujenzi huo






Chapisha Maoni

Mpya zaidi Nzee zaidi