Na: Tabu Shaibu
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais
Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jaffo amekagua maandalizi ya ujenzi wa
Barabara ya Mnyamani hadi Vingunguti na kusema kuwa ameridhika na maandalizi ya
ujenzi wa barabara hiyo. Mhe Jaffo
alifanya ukaguzi huo tarehe 23/01/2018 ikiwa ni takribani majuma mawili yamepita tangu alipoitembelea
barabara hiyo na kujionea ubovu uliokuwepo. Katika Maagizo yake aliyoyatoa aliitaka
Manispaa ya Ilala, Wakala wa Barabara Mjini na Vijijini na DAWASCO kushirikiana
pamoja na kuhakikisha kuwa Barabara hiyo inajengwa upya ili kuondokana na kero
iliyokuwa ikisababishwa na ubovu wa barabara hiyo.
Aidha Mhe Jaffo ameelekeza kuwa Mkandarasi atakeyetekeleza
kazi hiyo ahakikishe anatekeleza katika muda unaotakiwa kwa viwango bora. Kwa upande
wake Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe. Sophia Mjema ambaye aliongozana na Mhe Jaffo katika ukaguzi
wa maandalizi hayo amewakikishia wananchi wa maeneo ya Buguruni na Vingunguti
kuwa Serikali itaendelea kusimamia ahadi zake ili kila mwananchi aweze kuishi
maisha bora yenye kuinua uchumi wao.