Madiwani wa Ilala Waapishwa katika ukumbi wa Anatoglou

 Na Mariam Hassan

Katika ukumbi wa Anatoglou wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala leo mapema asubuhi kumefanyika  Uzinduzi wa baraza la Madiwani pamoja na uapishwaji wa Madiwani.



Baraza hilo liliongozwa na Mwenyekiti Katibu Tawala Wilaya ya Ilala Bi.Charangwa Selemani aliwapongeza madiwani kwa kuchaguliwa tena na kuwasisitiza kutimiza ahadi zao walizowaahidi wananchi.

Hakimu Mkazi Mahakama Kuu  ya Sokoine Drive Mh. Aziza Kalli aliongoza zoezi la uapishaji madiwani wote, na pia madiwani walifanya uchaguzi wa Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala ambaye aliyechaguliwa ni Mh. Omary Kumbilamoto diwani wa Kata ya Vingunguti aliyepita kwa kura zote asilimia 100%, pia walifanya uchaguzi wa Naibu Meya ambaye aliyechaguliwa ni Mh. Saady Khimji diwani wa Kata ya Ilala naye alipita kwa kura zote asilimia 100%.


                                                                            Baadhi ya Madiwani wakila kiapo







                           Mbunge wa Ukonga Mh. Jerry Silaa akisikiliza kwa makini


Aidha, Mstahiki Meya Mh. Omary Kumbilamoto alitoa shukurani zake kwa madiwani wenzake kwa kumchagua kushika nafasi hiyo na kuwaahidi kuwa atashirikiana nao kwa kila shughuli ili kuleta maendeleo katika Manispaa ya Ilala, naye Naibu Meya Mh. Khimji alitoa shukurani zake kwa madiwani na kuahidi kushirikiana nao pamoja na Mstahiki Meya na Mkurugenzi ili kuleta maendeleo katika Manispaa.



           Mh. Omari Kumbilamoto ambae alichaguliwa kuwa Meya akitoa neno la shukrani



Pamoja na hayo madiwani waliunda Kamati za kudumu na kuchagua wenyeviti na wajumbe wa kamati hizo.

Katika kikao hicho cha Baraza la madiwani wananchi kutoka sehemu mbali mbali pamoja na Mashirika Binafsi walihudhuria.



                          Baadhi ya Wananchi waliofika katika ukumbi wa Anatoglou

Chapisha Maoni

Mpya zaidi Nzee zaidi