Mhe. Nderiananga azihimiza Halmashauri kutoa mikopo kwa wakati

 Na: Hashim Jumbe

Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Watu wenye ulemavu) Mhe. Ummy H. Nderiananga amezihimiza Halmashauri zote nchini kutoa kwa wakati mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na wenye ulemavu ili kuwarahisishia kuendesha biashara zao.

Hayo ameyasema leo katika ukumbi wa mikutano wa Arnatouglou uliopo Manispaa ya Ilala katika kikao kazi na Maafisa Ustawi, Maafisa Maendeleo na Maafisa Vijana wa Halmashauri zote za Jiji la Dar es Salaam

"Dhamira na nia ya Serikali ni njema sana kwa kundi la watu wenye ulemavu, vijana na wanawake na mwanzoni mnakumbuka ilikuwa wanawake 5% na vijana 5%, Serikali ikaja ikafanya maboresho ikasema sasa tunaweka wanawake 4%, vijana 4% na walemavu 2%, hapa ninachoona kwa pamoja tukishirikiana kama ambavyo tulivyoanzia 0% mpaka asilimia fulani tuendelee kuongeza kasi"

Aidha, Mhe. Nderiananga aliwahimiza watumishi hao kurahisisha upatikanaji wa mikopo kwa makundi hayo huku akisisitiza lengo la Serikali ni kuwaletea maendeleo wananchi wake "Maafisa Maendeleo, Maafisa Ustawi na Maafisa Vijana tusaidiane ili tuweze kurahisisha upatikanaji wa mikopo ili vikundi vingi na watu wengi wenye uhitaji kunufaika na mikopo hii"









Chapisha Maoni

Mpya zaidi Nzee zaidi