- lengo ni kubaini barabara na madaraja yaliyoathirika na mvua zinazoendelea
- maagunia aina ya kisalfet yaliyojazwa michanga yasaidia kutengeneza vivuko vya dharura
Na:
Lucy Semindu Ilala
Kamati
ya mipango miji na mazingira ya Halmashauri ya Manispaa ya Ilala jana ilifanya
ziara katika maeneo mbalimbali ya Manispaa ya Ilala kubaini barabara
zilizoathirika na mvua.
Mwenyekiti
wa Kamati ya Mipango Miji na Mazingira Mhe. Sultan Salim aliiongoza kamati yake
katika maeneo hayo. Kata ziizotembelewa ni Kata za Chanika,Pugu ,Majohe ,Gongo la
mboto, Ukonga, Kivule na Kata ya Kitunda.
Katika
Kata ya Majohe Diwani wa Kata hiyo Mhe. Green Chilambo aliwaongoza wajumbe wa
Kamati ya Mipango miji katika maeneo mbalimbali ya Kata yake. Mhe. Chilambo
aliieleza kamati kuwa katika Mtaa wa Kichangani watu watatu walifariki dunia
baada ya nyumba yao kujaa maji wakati wakiwa wamelala.
Pia alisema kuwa katika Kivuko cha kwa Edward
ambacho kinaunganisha Kigogo fresh na eneo la Shule ya Msingi na Zahanti ya
Majohe, mama mmoja kwa bahati mbaya alishindwa kuokoa mtoto wake mdogo ambaye
alikufa baada ya kuchukuliwa na maji.
Maeneo
mengine yaliyoathirika katika Kata hiyo ni Mtaa wa Kichangani kwa Ngozoma eneo
la kwa Mzee Piro ambapo Nyumba 200 zimezungukwa na maji, barabara ya Msongola mpaka Mtumbo, Mfereji kwa Dihoma ambao umekatika na kuachanisha barabara inayotoka Pugu Sekondari
kuelekea Majohe na pia kipande cha barabara
kinachotoka Pugu Sekondari hadi Reli ya Tazara kuelekea Majohe kimeharibika.
Aidha,
Kamati hiyo ilishuhudia jinsi mvua kubwa zilizonyesha mwezi huu zilivyoharibu
barabara, madaraja, vivuko na mifereji. Katika Kata ya Chanika barabara
iliyounganisha Taliani na Vikongoro ilikuwa imeaharibika sana kwani wakazi wa
maeneo hayo imekuwa vigumu kuwasiliana kutokana na jinsi barabara hizo zilivyoharibika.
Mwenyekiti
wa Mtaa wa Vikongoro Bw Seif Mwera, aliieleza
kamati kuwa nyakati za mvua imekuwa vugumu hasa kwa wagonjwa kuweza kupelekwa
kwenye zahanati kwani kuharibika kwa barabara kimekuwa kikwazo kwa wananchi wa eneo hilo
kupata huduma muhimu.
Nalo
Daraja la Kimwani linalounganisha Msumbiji na Nzasa lilikuwa limevunjika. Mkazi
wa eneo hilo Bi Mwajuma Shabani alisema kuwa imekuwa vigumu kupata mahitaji mbalimbali
ya kibinadamu kwa kuwa maeneo hayo hayafikiki kirahisi.
Kwa
upande wake Diwani wa Kata ya Chanika Mhe. Abdilahi Mpate ameeleza kuwa tathmini
iliyofanyika imeonesha Kata yake imeathitika sana na mvua zinazoendelea
kunyesha na kwamba ipo haya hatua za haraka zichukuliwe ili kurudisha
mawasilano kati ya maeneo mbalimbali ya Kata yake.
Naye
Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala Mhe. Jerry Silaa ambaye ni
Diwani wa Kata ya Gongo la Mboto aliionyesha kamati ya mipango miji jinsi Kata
yake ilivyoathirika na mvua hizo. Maeneo yaliyoathirika sana katika Kata hiyo
ni, Daraja la Kiltex ambapo tuta la barabara limeondoka na barabara nzima inayoelekea kiltex imeharibika
vibaya.
Kamati
pia ilikagua katika Kata ya Ukonga na kubaini barabara mbalimbali za Kata hiyo
jinsi zilivyoharibika vibaya. Maeneo yaliyoathirika sana ni barabara iendayo
Ulongoni.
Aidha
kamati hiyo ilikagua barabara za Kata ya Kivule ambapo Diwani wa Kata hiyo Mhe.
Nyansika Motena aliionyesha kamati ya mipango miji jinsi daraja la Kivule lilivyokatika.
Hata hivyo ilionekana jinsi wakazi wa
eneo hilo walivyojaza mifuko ya aina ya kisalfet mishanga na kutengeneza kivuko
cha dharula ambacho kimesaidia kuunganisha wakazi wa eneo hilo na maeneo
mengine ya Jiji la Dar es Salaam.
Eneo
la Mwisho kutembelewa lilikuwa ni Kata ya Kitunda ambapo Mhe. Mwalimu Daniel aliwaongoza wajumbe wa Kamati
ya Mipango miji. Barabara zilizoonekana zimeharibika vibaya ni Darala la
Magole, eneo la Pemba beach ambapo makazi ya watu yamezingirwa na maji na
barabara ya Nyantira -Kipera ambayo imejaa mashimo makubwa.
Halmashauri
ya Manispaa ya Ilala kupitia Kamati ya Mipango miji na mazingira imekuwa katika
shughuli zake za kila siku ikijitahidi kupanga na kusimamia utekelezaji wa miradi mbalimbali ya barabara, madaraja na
vivuko ambayo imekuwa ikitekelezwa kwa kiwango kikubwa ili mawasiliano na
usafiri katika Manispaa ya Ilala yawezwe
kuboreshwa.
Kuharibika
kwa barabara kulikotokana na athari za mvua ni changamoto kubwa kwa kamati
hiyo. Ziara ya Kamati ya Kamati ya
mipango miji na mazingira inaendelea leo katika Kata nyingine zilizoathirika na
mvua.