Halina mada


WAFANYABIASAHARA WAKAIDI ILANI ILIYOTOLEWA NA HALMASHAURI YA MANISPAA YA ILALA

·        WAJENGA UPYA VIBANDA VILIVYOBOLEWA

Na Lucy Semindu – Vingunguti

Wafanyabiashara wa Vingunguti wakaidi amri halali ya Halmashauri ya Manispaa ya Ilala, iliyowataka wabomoe vibanda vya biashara vilivyojengwa katika maneo yasiyorusiwa. Hayo yameonekana wazi baada ya Manispaa ya Ilala kubomoa vibanda hivyo tarehe 14 aprili 2014 na wafanyabiashara hao kuvijenga upya tena.

Hali imeifanya Manispaa ya Ilala kwenda leo kwa mara nyingine kuvibomoa vibanda hivyo. Katibu Tarafa wa Ilala bibi Christina Kalekezi amesema ameshangazwa na kitendo kilichofanywa na wafanyabisahara hao kwani wamekaidi amri iliyotolewa na Halmashauri ya Manispaa ya Ilala.

Kikosi cha Jeshi la Polisi na la Mgambo kilionekana leo katika maeneo ya Vingunguti relini, Machinjio ya Vingunguti na katika Reli iliyopo Buguruni kwa myamani wakivunja vibanda vya wafanyabiashara vilivyojengwa katika maeneo yasiyoruhusiwa.

Hata hivyo ilionyesha wazi kuwa walikwisha tangaziwa  kuviondoa vibanda hivyo, kwani sehemu nyingi bidhaa zilikuwa zimekwishaondolewa katika vibanda. Mfanyabiashara wa relini njia ya kwa mnyamani ambaye jina lake halikuweza kufahamika mara moja, aliwashangaza wengi pale kijiko cha Manispaa kilipotaka kuvunja kibanda chake.

Mfanyabiashara huyo alianza kutweta na kusaidiwa na ndugu na jamaa zake kuondoa rundo la nguo zilizokuwa zimejaa kwenye kibanda chake. Hata hivyo shughuli zilisimama kwa takriban dakika kumi na tano ili aweze kuondoa nguo zote zilizokuwemo katika kibanda hicho cha biashara .

Naye Ndugu Joseph Manento amesifu sana zoezi hilo kwani sasa jiji ni safi na karibu sehemu nyingi zinapitika kirahisi. Ameomba jitihada hizi za kurudisha hadhi jiji la Dar es Salaam liendelee.


Kwa upande wake Katibu Tarafa wa Kariakoo Bw. M. Muyenjwa  amesema kuwa zoezi hili linaendelea na ni la kudumu kwani jiji la Dar s Salaam linatakiwa liwe ni sehemu salama na safi. Imekuwa ni desturi kwa wafanyabiashara kukaidi matangazo yanayotolewa ipo haja wakazingatia maelekezo wanayopewa. 


                                               Vibanada vikivunjwa katika eneo la vingunguti relini.



                                      Greda likiwa katika harakati la kuvunja vibanda        






                                         wananchi wakiambiwa kutawanyika ili  kuruhusu kazi inedelee vizuri

                                                          ( Picha zote na: Lucy Semindu )







Chapisha Maoni

Mpya zaidi Nzee zaidi