GIRL GUIDES TANZANIA WAPATA WANACHAMA WAPYA 117 SHULE YA WASICHANA UHURU




Na David Langa.
Girl guides ni chama cha hiari kinacholenga kuwajengea watoto wa kike na wasichana uwezo wa kujiamini, kujitegemea, kuitolea na kuwa na maadili na heshima mbele ya jamii nzima. Nchini Tanzania kuna zaidi ya watoto wa kike na wasichana zaidi  ya laki 2 ambao ni wanachama hai wa  wa chama hiki.
Wiki hii chama hiki kimewaingiza jumla ya wanachama wapya 117 katika  shule pekee ya wasichana nchini Tanzania ya Uhuru  iliyopo Manispaa ya Ilala  jijini Dar Es Salaam. Wanachama hawa wapya wamkefikia hatua hiyo baada ya kuhitimu mafunzo ya miezi sita yaliyokuwa yakiendeshwa na wakufunzi katika shule hiyo ambapo wahitimu walivyalishwa beji ya uanachama pamoja na kula kiapo cha utii mbele ya mgeni rasmi.

Moja ya kiapo cha wanachama hao wapya ni kuhakikisha kila siku kabla ya kulala kutenda jambo moja au zaidi la wema au kujitolea kusaidia jamii.


Sehemu ya wanachama wapya  wa shule ya msingi ya wasichana Uhuru wakisubiri kuapishwa

Viongozi na walenzi wa chama cha Girls guide wakitoa maelezo kwa wanachama wapya kabla ya kuwaapisha

Mkufunzi wa kitaifa wa chama hicho Bi. Expencer Violet Siame akiwaapisha wanachama wapya na kuwapa ahadi muhimu za chama .

Mdhamini wa chama cha Girl guides nchini Tanzania tangu mwaka 1965 Bi.Siami Mohamed akimvisha taji mwanachama mpya baada ya kula kiapo cha utii


Chapisha Maoni

Mpya zaidi Nzee zaidi