KAMATI NDOGO YA VIBALI VYA UJENZI MANISPAA YA ILALA YAFANYA ZIARA YA UKAGUZI WA VIBALI MAENEO YA PEMBEZONI MWA MJI

Na: Hashim Jumbe
Kamati ndogo inayosimamia vibali vya ujenzi Manispaa ya Ilala ikiongozwa na Mwenyekiti wake Mh.Sultan Salim, imefanya ziara ya siku moja ya ukaguzi wa vibali vya ujenzi katika maeneo ya pembezoni mwa mji.
Kamati hiyo ilitembelea eneo la Pugu Kinyamwezi na kukagua ujenzi wa ghorofa linalojengwa na Kampuni ya KAMAKA na kubaini mapungufu makubwa katika ujenzi huo ikiwemo kubadilisha matumizi ya kibali cha ujenzi kutoka kibali cha ujenzi wa ghala la kuhifadhia bidhaa na kutumia kibali hicho kwa ujenzi wa ghorofa.
Kamati hiyo pia ilitembelea na kukagua ujenzi wa jengo la hospitali ya kujifunzia kwa vitendo la Chuo kikuu cha Kampala kilichopo Gongolamboto, na kubaini mapungufu katika ujenzi huo yakiwemo ya kukosekana kwa kibali cha ujenzi na kibali cha tathmini ya mazingira huku ujenzi huo ukiendelea kufanyika katika eneo hatarishi.

Kamati hiyo imesimamisha ujenzi wa jengo la KAMAKA na ujenzi katika Chuo kikuu cha Kampala hadi hapo utaratibu wa ujenzi utakapokua umefuatwa.

Wajumbe wa Kamati ndogo ya Vibali vya Ujenzi Manispaa ya Ilala wakifanya ukaguzi katika jengo linalomilikiwa na Kampuni ya KAMAKA eneo la Pugu Kinyamwezi

Naibu Meya wa Manispaa ya Ilala ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati ndogo ya vibali vya ujenzi Mh. Kheri Kessy akiongea na fundi aliyekua akijenga ghorofa ya KAMAKA



Eneo hatarishi kwa ujenzi likiwa limeanza kujengwa msingi wa jengo la hospitali ya kujifunzia katika chuo Kikuu cha Kampala tawi la Gongolamboto


Chapisha Maoni

Mpya zaidi Nzee zaidi