TANGAZO LA LESENI ZA VILEO


 

                              
                     HALMASHAURI YA MANISPAA YA ILALA


 
 

TANGAZO

MAOMBI YA LESENI ZA VILEO KWA KIPINDI KINACHOANZIA TAREHE 01 APRIL, 2015 NA KUISHIA TAREHE 30 SEPTEMBA, 2015

Chini ya Sheria ya Leseni za Vileo Na. 28 ya 1968 na marekebisho yake sehemu 1V kifungu 38(1) – (4) na 39 (1-3).

 

Wafanyabiashara wote wanaoendesha Biashara ya Vileo katika Manispaa ya Ilala wanatangaziwa kwamba Fomu za maombi ya Leseni za Vileo kwa kipindi kitakachoanza tarehe 01/O4/2015 na kuishia tarehe 30/09/2015 zinaanza kutolewa kuanzia tarehe 16/03/2015.

 

Fomu za maombi ya Leseni za Vileo zinapatikana katika Ofisi ya Biashara Manispaa ya Ilala, katika Jengo la Arnatoglou karibu na Hospitali ya Mnazimmoja.

 

Fomu za maombi ya zamani (Renewals) zijazwe kikamilifu na kurejeshwa Ofisi ya Biashara ya Manispaa ya Ilala, ziambatanishwe na kivuli (Photocopy) cha Leseni ya kipindi kinachoishia tarehe 31/03/2015 pamoja na TIN, pia fomu ipitishwe kwa Mwenyekiti wa Kamati ya maendeleo ya Kata husika.

 

Fomu za maombi mapya zipitishwe ngazi zote kama zilivyooneshwa kwenye kifungu na 9 (tisa) kabla hazijarejeshwa katika Ofisi ya Biashara.

 

Maombi yote yawasilishwe kwa Afisa Biashara kabla ya tarehe 01/ April, 2015  limetolewa na:-

 

 

Isaya M. Mngurumi

MKURUGENZI WA MANISPAA

HALMASHAURI YA MANISPAA YA ILALA.

Chapisha Maoni

Mpya zaidi Nzee zaidi