MANISPAA YA ILALA YA ADHIMISHA SIKU YA ELIMU NA KILELE CHA UBORESHAJI WA MAZINGIRA KATIKA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI

Na: Hashim Jumbe
Idara ya Elimu Msingi na Elimu Sekondari Manispaa ya Ilala, wameadhimisha siku ya elimu (Elimu Day) na kufikia kilele cha uboreshaji wa mazingira kwa Walimu na Wanafunzi wa shule za Msingi na Sekondari zilizopo Manispaa ya Ilala.
Maadhimisho hayo yaliyofanyika mwishoni mwa juma lililopita katika viwanja vya Mnazi Mmoja yaliwashirikisha Wadau mbalimbali wa elimu na mazingira wakiwemo Waratibu wa Clasta, Waratibu wa Elimu Kata, Wakuu wa Shule na Wanafunzi wa Shule za Msingi na Sekondari.
Aidha, maadhimisho hayo yaliambatana na utoaji wa zawadi mbalimbali zikiwemo vifaa vya usafi, vikombe vya ushindi na vyeti kwa Walimu na Wanafunzi waliofanya vizuri katika taaluma na usafi wa mazingira.
Akitoa wito kwa Wananchi wanaoishi Manispaa ya Ilala pamoja na asasi zote, Idara na sekta za Umma, Mgeni Rasmi wa Maadhimisho hayo Mh. Raymond Mushi ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Ilala amewataka kuhakikisha suala la Elimu ya Mazingira na Usafi linapewa  kipaumbele katika maeneo yao. “Kila mmoja kwa nafasi yake anatakiwa ashiriki kikamilifu katika  kuhifadhi  mazingira kulingana na Sheria  zilizopo zinavyoelekeza. Nasisitiza,  kuwa Maafisa Mazingira na Mabwana Afya  katika ngazi mbali mbali kufanya kazi kwa bidi”.


Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Jangwani wakiandamana kupita mbele ya mgeni rasmi wakati wa maadhimisho ya siku ya elimu na kilele cha uboreshaji wa mazingira huku wakiwa na bango linalosomeka “Elimu bora, kwa mazingira bora”
    Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Mh. Raymond Mushi ambaye pia ni Mgeni rasmi katika maadhimisho ya siku ya elimu na kilele cha uboreshaji wa mazingira, akiangalia mchezo wa mpira wa mezani(table tennis) uliokua ukichezwa na Wanafunzi wenye ulemavu kutoka shule ya Sekondari ya Pugu.

   Mwanafunzi aliyeshika nafasi ya kwanza katika mitihani ya kumaliza elimu ya
kidato cha Nne mwaka 2014 kwa shule za Manispaa ya Ilala aliyetokea shule ya Sekondari Shaaban Robert akipokea zawadi ya cheti kutoka kwa Mgeni rasmi. 


    Diwani wa Kata ya Ilala Mh. Edson Fungo mwenye shati jekundu akifurahia pamoja na Walimu na Wanafunzi wa shule ya Msingi Msimbazi Mseto baada ya kukabidhiwa kikombe cha ushindi kwa kushika nafasi ya kwanza katika mitihani ya kumaliza elimu ya msingi mwaka 2014 kwa shule za Serikali za Manispaa ya Ilala



 Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala, Ndugu Issaya Mngurumi,aliyepo kushoto akimkabidhi Mgeni Rasmi zawadi iliyotolewa na Walimu kwa kuthamini mchango wake katika sekta ya elimu

 Walimu na Wanafunzi wa shule ya Tusiime wakishangiria ushindi wa jumla walioupata katika maadhimisho ya siku ya elimu na kilele cha uboreshaji wa mazingira kwa mwaka 2015. 



Afisa Elimu Msingi Manispaa ya Ilala Bi. Elizabeth Thomas akicheza ngoma aina ya makhirikhiri pamoja na Wanafunzi kutoka shule ya msingi Umoja kutoka Kiwalani









Chapisha Maoni

Mpya zaidi Nzee zaidi