KODI YA MAJENGO, LESENI ZA BIASHARA NA KODI YA HUDUMA ZA JIJI

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala anawatangazia Wakazi pamoja na Wamiliki wote wa majengo katika Manispaa ya Ilala kuwa, siku ya mwisho ya kulipia kodi ya majengo kwa mwaka wa fedha wa 2014/15 ni tarehe 30 Juni, 2015.  Wote ambao hawajalipia majengo yao wahakikishe kuwa wanalipa kabla ya tarehe ya mwisho. Wafanyabishara wahakikishe wamelipia Leseni zao na Ushuru wa Huduma za Jiji. Wote watakaochelewa kulipa  watachukuliwa hatua za kisheria ikiwa ni pamoja na kutozwa faini ya asilimia 25 ya kodi anayastahili kulipa.
Lipa kodi kwa wakati kuepuka usumbufu.

Limetolewa na,

ISAYA M. MNGURUMI
MKURUGENZI WA MANISPAA,

HALMASHAURI YA MANISPAA YA ILALA

Chapisha Maoni

Mpya zaidi Nzee zaidi