DC-MJEMA AKABIDHI GARI YA KUBEBEA WAGONJWA HOSPITALI YA CHANIKA NA KISHA AWAJULIA HALI WAMAMA WALIOJIFUNGUA

Na: Hashim Jumbe
Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Mhe. Sophia Mjema amekabidhi gari ya kubebea Wagonjwa kwenye Hospitali ya Mama na Mtoto Chanika (Korea-Tanzania Friendship Maternity Hospital). Gari hiyo yenye thamani ya Shilingi Milioni 140 limenunuliwa kutoka kwenye Mapato ya ndani ya Halmashauri ya Manispaa ya Ilala.

Makabidhiano ya gari hilo la Wagonjwa yanakamilisha mahitaji yote muhimu katika Hospitali hiyo ya Mama na Mtoto baada ya uwepo wa vifaa tiba, nyumba ya Watumishi pamoja na uwepo wa Watumishi wenyewe.

Wakati wa kukabidhi gari hiyo, Mhe. Sophia Mjema alipata pia fursa ya kukagua shughuli zinavyoendelea hospitalini hapo na kisha kusalimiana na Wamama waliojifungua.








Chapisha Maoni

Mpya zaidi Nzee zaidi