MANISPAA YA ILALA YAENDESHA MAFUZO YA SERA YA UWEZESHAJI WANANCHI KIUCHUMI KWA MADIWANI NA WAKUU WA IDARA

Na  Neema Njau

Halmashauri ya Manispaa ya Ilala kupitia dawati la uwezeshaji Wananchi kiuchumi leo imeendesha mafunzo ya Sera ya Taifa ya Uwezeshaji Wananchi kiuchumi ya mwaka 2004.

Akifungua mafunzo hayo Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala Mhe Charles B. Kuyeko ameeleza kuwa lengo la mafunzo hayo nikuwajengea uwezo Viongozi juu ya sera ,mkakati na mwongozo wa utekelezaji mkakati wa Taifa wa uwezeshaji wananchi kiuchumi ili wakaweze kuhamasisha wananchi kuwekeza na kujiwezesha kiuchumi.

Mada zilizojadiliwa.
i. Sera ya Uwezeshaji , Mkakati na Mwongozo  wa Utekelezaji
ii. Baraza , Majukumu na Programu zake
iii. Majukumu ya madawati na kamati za uwezeshaji ngazi ya Halmashauri, Kata na Mitaa
iv. Mifuko ya uwezeshaji wananchi kiuchumi
v. Taarifa za uwezeshaji wananchi kiuchumi.
Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala Mhe. Charles B. Kuyeko akifungua Mafunzo ya sera ya uwezeshaji Wananchi kiuchumi katika Ukumbi wa Arnatoglou uliopo Manispaa ya Ilala
Mratibu wa Dawati la Sera ya Uwezeshaji Wananchi kiuchumi Bibi Regina Ng'ong'olo akitoa mada katika mafunzo hayo

Baadhi ya Waheshimiwa Madiwani wakifuatilia mafuzo ya Sera ya uwezeshaji wananchi Kiuchumi katikaUkumbi wa Arnatoglou

Waheshimiwa Madiwani wakifuatilia mafuzo 

Wakuu wa Idara wakifuatilia mafunzo ya sera ya uwezeshaji wa Wananchi kiuchumi


Afisa Maendeleo ya Jamii  Bw. Barnabas Kisai akitoa mada wakati wa mafunzo hayo.

 Mwenyekiti wa Mafunzo ya Sera ya uwezeshaji Wananchi kiuchumi Mhe. Edwin Mwakatobe  Diwani Kata ya Segerea akitoa maelekezo kwa wajumbe wakati wa mafunzo hayo

Chapisha Maoni

Mpya zaidi Nzee zaidi