TAMKO LA HALMASHAURI YA MANISPAA YA ILALA

Halmashauri ya manispaa ya Ilala kupitia kikao chake cha Baraza cha tarehe 12/9/2014 imepiga marufuku vitendo vinavyofanywa na halmashauri ya jiji la Dar es salaam na mawakala wake wa Tambaza auction mart na askari wa jeshi la polisi kuwakamata wananchi wenye magari ya mizigo ya chini ya tani tatu na robo na kuwakatia vibali vya shilingi 500,000 kwa mwaka kinyume cha sheria.

Akisoma tamko hilo, mstaiki meya wa manispaa ya ilala Mhe.Jerry Silaa amesema halmashauri ya manispaa ya Ilala ndio yenye ardhi na sheria ndogo ya barabara inayoruhusu magari ya mizigo yasiyozidi tani tatu na robo kuingia mjini bila usumbufu wowote. Kitendo cha halmashauri ya jiji kutumia sheria ndogo za iliyokuwa tume ya jiji ambayo wanajua wazi ilivunjwa ni kuwaibia na kuwanyanyasa wananchi na kuwanyima kufanya shughuli zao za kiuchumi.

 

Baraza la madiwani linamtaka IGP ernest Mangu awaagize mara moja askari wake waache kushirikiana na mawakala kuwanyanyasa wananchi kwa kutumia sheria zilizofutwa na kubaka eneo la utawala la halmshauri ya manispaa ya ilala. Na aagize vituo vyake vya polisi kutotumika kuwaweka rumande wananchi bila msingi wa sheria.

 

Vilevile halmashauri inamtaka msajili wa mahakama kuiagiza mahakama ya jiji kutotumika kuwatoza faini wananchi na wakati mwengine kuwaweka rumande.

 

Halmashauri ya Manispaa ya Ilala inawataka wananchi waendelee kuzingatia sheria ndogo ya barabara ya halmashauri ya manispaa ya Ilala na wanapokamatwa na mtu yeyote wadai kuonyeshwa sheria inayotumika au kufika ofisi ya mkurugenzi wa halamshauri ya manispaa ya Ilala kwa ufafanuzi zaidi.

 

1 Maoni

Mpya zaidi Nzee zaidi