KAMATI YA BUNGE YATEMBELEA ILALA.

 
Na David Langa
Kamati ya Bunge Hesabu za serikali za mitaa LAAC  inayoongozwa  na Mh. Rajab Mbarouk  (MB) imetembelea Manispaa ya Ilala na kukagua mapato na matumizi kwa kipindi cha  mwaka 2012/2013 ambapo pamoja na mambo mengine walitembelea miradi mbalimbali iliyotekelezwa kwa kipindi hicho.
Akitoa ufafanuzi juu ya hali halisi ya Manispaa kwa kipindi hicho, Meya wa Manispaa ya Ilala Mh. Jerry Silaa alisema kwa kipindi hicho Manispaa imeweza kukusanya zaidi ya shilingio Bilioni 25 na kutekeleza miradi mbalimbali ikiwemo ujenzi wa madarasa, barabara, vyoo vya wanafunzi, ujenzi wa zahanati pamoja na ununuzi wa madawati zaidi ya 13,000 kwa shule za msingi.
Kwa upande wake Mgurugenzi wa Manispaa Ndg Isaya Mngurumi amesema Manispaa imepanga kutekeleza miradi mbalimbali ya kijamii pamoja na kutenga shilingi milioni 700 kwa ajili ya mfuko wa vijana na akina mama itakayotolewa kama mkopo kwa wananchi kupitia benki ya wananchi wa Dar  es salaa (DCB)
 
 
 
Mkuu wa Mkoa wa Dar Es salaam Mh. Mecky Sadick  akimkaribisha mwenyekiti wa kamati ya Bunge Hesabu za serikali za mitaa Mh. Rajabu Mbarouk na kamati yake katika ukumbi wa mikutano ya Anatoglou .

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala Bw. Isaya Mngurumi akijibu baadhi ya hoja zilizojitokeza katika mjadala kati yaa kamati ya Bunge na kamati ya fedha na utawala wa manispaa ya Ilala. kushoto kwake ni Mstahiki meya wa Manispaa ya Ilala Mh. Jerry Silaa.

mwenyekiti wa Kamtri ya Bunge Hesabu za serikali za Mitaa Mh. Rajabu Mbarouk akiongea katika mkutano huo ndani ya ukumbi wa Anatoglou  Ilala jiji Dar es salaam

kamati ya Bunge walipotembelea ujenzi wa ofisi ya kata ya Kivule iliyojengwa kwa fedha za ndani

mtendaji wa kata ya Kivule akitoa maelezo kwa kamati kwa kamati juu ya ujenzi wa ofisi hiyo iliyogarimu zaidi ya milioni 100,.

ANkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala Bw. Isaya Mngurumi akiwatembeza wajumbe wa kamati ya Bunge LAAC kukagua ofisi ya kata ya Kivule


Mkuu wa Wilaya ya  ilala (kulia) akiwaongoza kamati ya Bunge walipotembelea sokpo la samaki Ferry ambalo ni moja ya miradi ya  Halmashauri ya Manispaa ya Ilala.

wajumbe ndani ya soko la Ferry .

Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala Mh. Jerry Silaa akiongea na vijana wafanyabiashara wa samaki wa soko la Ferry.

Chapisha Maoni

Mpya zaidi Nzee zaidi