Na:
Hashim Jumbe, kutokea Zanzibar
Timu ya Madiwani wa Manispaa ya Ilala iliyoshiriki
tamasha la Pasaka visiwani Zanzibar lililoandaliwa na Halmashauri ya Wilaya ya
Mjini Magharibi imevuta hisia za wapenzi wa michezo visiwani hapa waliojitokeza
kwa wingi kuwashuhudia.
Katika mchezo wa ufunguzi wa tamasha hilo
uliofanyika katika viwanja vya Amani, timu ya mpira wa miguu ya Madiwani wa
Manispaa ya Ilala walipoteza mchezo wao kwa kukubali kufungwa magoli 3-2 na
wenyeji wao wa Wilaya ya Mjini Magharibi, licha ya kucheza soka safi na
lakuvutia lililowafanya kushangiliwa muda wote wa mchezo.
Aidha, tamasha hilo lilihusisha na michezo mingine
mbalimbali iliyochezwa kwenye fukwe za Kizimkazi kama vile michezo ya kuvuta
kamba, kukuna nazi, kukimbia na gunia, mbio za ufukweni na kukimbiza kuku.
Katika tamasha hilo ushindi wa jumla umekwenda kwa
Manispaa ya Ilala baada ya kufanya vyema kwenye mashindano ya ufukweni na
kupata kikombe na medali za shaba huku Mheshimiwa Tumike aking’ara kwenye
shindano la kukuna nazi, Mheshimiwa Mtumwa Mohamed akishika nafasi ya kwanza
kwa kukimbia na gunia.
Madiwani Wanawake wa Manispaa ya Ilala wakiongozwa na Hajjat Lai Ninga wakishiriki shindano la kuvuta kamba kwenye tamasha la Pasaka visiwani Zanzibar |
Diwani wa Kata ya Tabata(kulia) Mh. Mtumwa Mohamed akiongoza mbio za kukimbia na gunia kwa Madiwani Wanawake |
Diwani wa kata ya Ilala Mh. Edson Fungo akikuna nazi
katika shindano la kumtafuta mshindi wa kukuna katika fukwe za Kizimkazi
|
Mwenyekiti wa Kamati ya Uchumi na Huduma za Jamii Manispaa ya Ilala, Mh. Angelina Malembeka akimkabidhi kalenda za Manispaa ya Ilala Mwenyekiti wa Wilaya ya Mjini Magharibi |
safi sana wanailala kutuwakilisha vyema huko zenji
JibuFuta